Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:53-66 Biblia Habari Njema (BHN)

53. Wenye njaa amewashibisha mema,matajiri amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli mtumishi wake,akikumbuka huruma yake,

55. kama alivyowaahidia wazee wetu,Abrahamu na wazawa wake hata milele.”

56. Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.

57. Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.

58. Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.

59. Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakaria.

60. Lakini mama yake akasema, “Sivyo, bali ataitwa Yohane.”

61. Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”

62. Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.

63. Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.

64. Papo hapo, midomo na ulimi wake Zakaria vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.

65. Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.

66. Wote waliosikia mambo hayo, waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.

Kusoma sura kamili Luka 1