Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:52-58 Biblia Habari Njema (BHN)

52. amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi,akawakweza wanyenyekevu.

53. Wenye njaa amewashibisha mema,matajiri amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli mtumishi wake,akikumbuka huruma yake,

55. kama alivyowaahidia wazee wetu,Abrahamu na wazawa wake hata milele.”

56. Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.

57. Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.

58. Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.

Kusoma sura kamili Luka 1