Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:46-52 Biblia Habari Njema (BHN)

46. Naye Maria akasema,“Moyo wangu wamtukuza Bwana,

47. roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.

48. Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu.Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.

49. Kwa kuwa Mungu Mwenye Nguvu amenifanyia makuu,jina lake ni takatifu.

50. Huruma yake kwa watu wanaomchahudumu kizazi hata kizazi.

51. Amefanya mambo makuu kwa mkono wake:Amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

52. amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi,akawakweza wanyenyekevu.

Kusoma sura kamili Luka 1