Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:44-62 Biblia Habari Njema (BHN)

44. Nakuambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.

45. Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokuambia.”

46. Naye Maria akasema,“Moyo wangu wamtukuza Bwana,

47. roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.

48. Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu.Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.

49. Kwa kuwa Mungu Mwenye Nguvu amenifanyia makuu,jina lake ni takatifu.

50. Huruma yake kwa watu wanaomchahudumu kizazi hata kizazi.

51. Amefanya mambo makuu kwa mkono wake:Amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

52. amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi,akawakweza wanyenyekevu.

53. Wenye njaa amewashibisha mema,matajiri amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli mtumishi wake,akikumbuka huruma yake,

55. kama alivyowaahidia wazee wetu,Abrahamu na wazawa wake hata milele.”

56. Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.

57. Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.

58. Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.

59. Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakaria.

60. Lakini mama yake akasema, “Sivyo, bali ataitwa Yohane.”

61. Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”

62. Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.

Kusoma sura kamili Luka 1