Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:39-46 Biblia Habari Njema (BHN)

39. Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yudea.

40. Huko, aliingia katika nyumba ya Zakaria, akamsalimu Elisabeti.

41. Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu,

42. akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.

43. Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?

44. Nakuambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.

45. Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokuambia.”

46. Naye Maria akasema,“Moyo wangu wamtukuza Bwana,

Kusoma sura kamili Luka 1