Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 1:29-36 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: Maneno hayo yanamaanisha nini?

30. Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.

31. Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu.

32. Yeye atakuwa mkubwa na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.

33. Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

34. Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”

35. Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.

36. Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.

Kusoma sura kamili Luka 1