Agano la Kale

Agano Jipya

2 Yohane 1:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.

11. Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.

12. Ninayo mengi ya kuwaambieni, lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.

13. Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.

Kusoma sura kamili 2 Yohane 1