Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wakorintho 6:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.

2. Mungu asema hivi:“Wakati wa kufaa nimekusikiliza,wakati wa wokovu nikakusaidia.”Basi, sasa ndio wakati wa kufaa; sasa ndiyo siku ya wokovu!

3. Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuizi chochote.

4. Badala yake, tunajionesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: Kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.

5. Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.

Kusoma sura kamili 2 Wakorintho 6