Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wakorintho 10:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mimi Paulo mwenyewe ambaye naonekana kuwa mpole nikiwa pamoja nanyi, lakini mkali niwapo mbali nanyi, nawasihini kwa huruma na wema wake Kristo.

2. Nawaombeni msinisababishe kuwa mkali wakati nitakapokuja, maana nina hakika naweza kuwa mkali kwa wote wale wanaotudhania kwamba tunaishi kidunia.

3. Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia.

4. Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu ya Mungu yenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo

Kusoma sura kamili 2 Wakorintho 10