Agano la Kale

Agano Jipya

2 Timotheo 2:22-26 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.

23. Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.

24. Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,

25. ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.

26. Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.

Kusoma sura kamili 2 Timotheo 2