Agano la Kale

Agano Jipya

1 Yohane 2:24-27 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.

25. Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: Uhai wa milele.

26. Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha nyinyi.

27. Lakini, kwa upande wenu nyinyi, Kristo aliwatia mafuta kwa Roho wake. Na kama Roho huyo akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana yeye anawafundisheni kila kitu, na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi, shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.

Kusoma sura kamili 1 Yohane 2