Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wathesalonike 5:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.

7. Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.

8. Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.

9. Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo

10. ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.

11. Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana nyinyi kwa nyinyi, kama mnavyofanya sasa.

12. Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.

Kusoma sura kamili 1 Wathesalonike 5