Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wathesalonike 5:15-23 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.

16. Furahini daima,

17. salini kila wakati

18. na kuwa na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.

19. Msimpinge Roho Mtakatifu;

20. msidharau unabii.

21. Pimeni kila kitu: Zingatieni kilicho chema,

22. na kuepuka kila aina ya uovu.

23. Mungu mwenyewe anayetupatia amani awatakase nyinyi kabisa kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu – roho, mioyo na miili yenu – mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Kusoma sura kamili 1 Wathesalonike 5