Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 9:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, nyinyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?

2. Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu nyinyi mimi ni mtume. Nyinyi ni uthibitisho wa utume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.

3. Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:

4. Je, hatuna haki ya kula na kunywa?

5. Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?

6. Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?

7. Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?

8. Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, sheria nayo haisemi hivyo?

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 9