23. Nyote mmenunuliwa kwa bei; kwa hiyo msiwe tena watumwa wa watu.
24. Ndugu zangu, kila mmoja wenu basi, na abaki na Mungu kama alivyokuwa wakati alipoitwa.
25. Sasa, kuhusu mabikira na waseja, sina amri kutoka kwa Bwana; lakini natoa maoni yangu mimi ambaye kwa huruma yake Bwana nastahili kuaminiwa.
26. Basi, kutokana na shida iliyopo sasa nadhani ingefaa mtu abaki kama alivyo.