Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 4:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. tukisingiziwa, tunajibu kwa adabu. Mpaka sasa tumetendewa kama uchafu wa dunia; na kwa kila mtu sisi ni takataka!

14. Siandiki mambo haya kwa ajili ya kuwaaibisha nyinyi, bali kwa ajili ya kuwafundisheni watoto wangu wapenzi.

15. Maana hata kama mnao maelfu ya walezi katika maisha yenu ya Kikristo, baba yenu ni mmoja tu, kwani katika kuungana na Kristo mimi ndiye niliyewazaeni kwa kuihubiri Habari Njema.

16. Kwa hiyo, nawasihi: Fuateni mfano wangu.

17. Ndiyo maana nimemtuma Timotheo kwenu. Yeye ni mtoto wangu mpenzi na mwaminifu katika kuungana na Bwana. Atawakumbusheni njia ninayofuata katika kuungana na Kristo; njia ninayofundisha kila mahali katika makanisa yote.

18. Baadhi yenu wameanza kuwa na majivuno wakidhani kwamba sitakuja tena kwenu.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 4