19. Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: “Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao.”
20. Na tena: “Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai.”
21. Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22. Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23. Lakini nyinyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.