19. Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priska pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika kuungana na Bwana.
20. Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21. Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22. Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANATHA – BWANA, NJOO!
23. Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24. Upendo wangu uwe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.