Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 15:30-36 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?

31. Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.

32. Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”

33. Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.

34. Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!

35. Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”

36. Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 15