Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 15:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.

3. Mimi niliwakabidhi nyinyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;

4. kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kufuatana na Maandiko Matakatifu;

5. kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.

6. Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya 500 kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.

7. Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.

8. Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 15