Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 15:11-22 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachohubiri, na hiki ndicho mnachoamini.

12. Sasa, maadamu inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?

13. Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;

14. na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.

15. Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka kwa wafu na kumbe yeye hakumfufua – kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.

16. Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.

17. Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.

18. Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.

19. Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.

20. Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, wa kwanza wa wale waliolala katika kifo.

21. Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka kwa wafu kumesababishwa na mtu mmoja.

22. Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 15