Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 15:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Sasa, ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni, nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.

2. Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.

3. Mimi niliwakabidhi nyinyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;

4. kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kufuatana na Maandiko Matakatifu;

5. kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 15