Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 14:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Kwa hiyo, mwenye kunena lugha ngeni na aombe apate uwezo wa kuzifafanua.

14. Maana, nikisali kwa lugha ngeni roho yangu ndiyo inayosali, lakini akili yangu hubaki bure.

15. Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.

16. Ukimsifu Mungu kwa roho yako tu, atawezaje mtu wa kawaida aliye katika mkutano kuitikia sala yako ya shukrani kwa kusema: “Amina”, kama haelewi unachosema?

17. Sala yako ya shukrani yaweza kweli kuwa bora, lakini huyo mwingine haitamfaidia.

18. Namshukuru Mungu kwamba mimi nasema kwa lugha ngeni kuliko nyinyi nyote.

19. Lakini katika mikutano ya waumini napendelea zaidi kusema maneno matano yenye kueleweka ili niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu ya lugha ngeni.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 14