Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 13:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mwenye upendo hakosi adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya,

6. hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.

7. Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.

8. Upendo hauna kikomo kamwe. Kama kuna vipaji vya kutangaza ujumbe wa Mungu, hivyo vitatoweka siku moja; kama ni vipaji vya kusema lugha ngeni, vitakoma; kama kuna elimu, nayo itapita.

9. Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 13