Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 12:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.

14. Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.

15. Kama mguu ungejisemea: “Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili,” je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!

16. Kama sikio lingejisemea: “Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili,” je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!

17. Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?

18. Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.

19. Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 12