Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 11:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.

9. Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.

10. Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.

11. Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.

12. Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 11