Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 11:27-31 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.

28. Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;

29. maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.

30. Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.

31. Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 11