Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 10:28-33 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.

29. Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni.Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?

30. Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”

31. Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.

32. Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.

33. Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 10