Agano la Kale

Agano Jipya

1 Petro 4:16-19 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi, asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.

17. Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi, mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?

18. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:“Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa;itakuwaje basi, kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?”

19. Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.

Kusoma sura kamili 1 Petro 4