Agano la Kale

Agano Jipya

1 Petro 3:9-16 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Msiwalipe watu ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi; bali watakieni baraka, maana nyinyi mliitwa na Mungu mpate kupokea baraka.

10. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:“Anayetaka kufurahia maisha,na kuona siku za fanaka,ajizuie asiseme mabayaaepe kusema uongo.

11. Ajiepushe na uovu, atende mema,atafute amani na kuizingatia.

12. Maana Bwana huwatazama kwa wema waadilifuna kuzisikiliza sala zao.Lakini huwapa kisogo watu watendao maovu.”

13. Ni nani atakayeweza kuwadhuru nyinyi kama mkizingatia kutenda mema?

14. Lakini, hata kama itawapasa kuteseka kwa sababu ya kutenda mema, basi, mna heri. Msimwogope mtu yeyote, wala msikubali kutiwa katika wasiwasi.

15. Lakini mtukuzeni Kristo kama Bwana mioyoni mwenu. Muwe tayari kumjibu yeyote atakayewaulizeni juu ya matumaini yaliyo ndani yenu,

16. lakini fanyeni hivyo kwa upole na heshima. Muwe na dhamiri njema, kusudi mnapotukanwa, wale wanaosema ubaya juu ya mwenendo wenu mwema kama Wakristo, waone aibu.

Kusoma sura kamili 1 Petro 3