Agano la Kale

Agano Jipya

1 Petro 2:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea tambiko za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.

6. Maana Maandiko Matakatifu yasema:“Tazama! Naweka jiwe huko Siyoni,jiwe la msingi, teule na la thamani.Mtu atakayemwamini huyo hataaibishwa.”

7. Kwenu nyinyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini,“Jiwe walilolikataa waashi,sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.”

8. Tena Maandiko yasema:“Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa,mwamba wa kuwaangusha watu.”Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.

Kusoma sura kamili 1 Petro 2