Agano la Kale

Agano Jipya

1 Petro 2:3-9 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.”

4. Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule na la thamani kubwa.

5. Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea tambiko za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.

6. Maana Maandiko Matakatifu yasema:“Tazama! Naweka jiwe huko Siyoni,jiwe la msingi, teule na la thamani.Mtu atakayemwamini huyo hataaibishwa.”

7. Kwenu nyinyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini,“Jiwe walilolikataa waashi,sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.”

8. Tena Maandiko yasema:“Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa,mwamba wa kuwaangusha watu.”Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.

9. Lakini nyinyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani, akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.

Kusoma sura kamili 1 Petro 2