Agano la Kale

Agano Jipya

1 Petro 2:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena.

2. Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.

3. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.”

4. Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule na la thamani kubwa.

Kusoma sura kamili 1 Petro 2