5. Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu,majaliwa yangu yamo mikononi mwako.
6. Umenipimia sehemu nzuri sana;naam, urithi wangu ni wa kupendeza.
7. Namsifu Mwenyezi-Mungu kwa kuniongoza,usiku dhamiri yangu yanionya.
8. Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima;yuko pamoja nami, wala sitatikisika.