19. “Je, Yobu, ndiwe uliyewapa farasi nguvu,ukawavika shingoni manyoya marefu?
20. Je, ni wewe unayemfanya farasi aruke kama nzige?Mlio wake wa maringo ni wa ajabu!
21. Huparapara ardhi mabondeni kwa pupa;hukimbilia kwenye mapigano kwa nguvu zake zote.
22. Farasi huicheka hofu, na hatishiki;wala upanga hauwezi kumrudisha nyuma.
23. Silaha wachukuazo wapandafarasi,hugongana kwa sauti na kungaa juani.