5. Nijibu, kama unaweza.Panga hoja zako vizuri mbele yangu,ushike msimamo wako.
6. Wewe na mimi ni sawa mbele ya Mungu;mimi pia niliumbwa kwa sehemu ya udongo.
7. Kwa hiyo huna sababu ya kuniogopa;maneno yangu mazito hayatakulemea.
8. Kweli umesema, nami nikasikia;nimeyasikia yote uliyosema.
9. Wewe umesema, u safi na wala huna kosa,u safi kabisa na huna hatia;
10. umesema kwamba Mungu anakutafutia kisa,na kukuona kama adui yake.
11. Anakufunga miguu minyororo,na kuchunguza hatua zako zote.
12. “Lakini Yobu, nakuambia hapo umekosea.Mungu ni mkuu kuliko binadamu.