27. Atashangilia mbele ya watu na kusema:‘Nilitenda dhambi na kupotosha haki,nami sikuadhibiwa kutokana na hayo.
28. Mungu aliniokoa nisiangamie Shimoni;nimebaki hai na ninaona mwanga.’
29. “Tazama Mungu humfanyia binadamu haya yote,tena mara mbili, mara tatu.
30. Humwokoa binadamu asiangamie Shimoni,aweze kuona mwanga wa maisha.
31. Sikia Yobu, nisikilize kwa makini;kaa kimya, nami nitasema.
32. Kama una la kusema, nijibu;sema, maana nataka kukuona huna hatia.
33. La sivyo, nyamaza unisikilize,kaa kimya nami nikufunze hekima.”