1. “Sasa, Yobu, sikiliza hoja yangu;sikiliza maneno yangu yote.
2. Tazama, nafumbua kinywa changu,naam, ulimi wangu utasema.
3. Nitasema kadiri ya unyofu wa moyo wangu;ninayoyajua nitayasema kwa uaminifu.
4. Roho ya Mungu iliniumba,nayo pumzi ya Mungu Mwenye Nguvu yanipa uhai.
5. Nijibu, kama unaweza.Panga hoja zako vizuri mbele yangu,ushike msimamo wako.