8. Wanyama waendao kwa madaha hawajazikanyagawala simba hawajawahi kuzipitia.
9. Binadamu huchimbua miamba migumu kabisa,huichimbua milima na kuiondolea mbali.
10. Hupasua mifereji kati ya majabali,na jicho lake huona vito vya thamani.
11. Huziba chemchemi zisitiririke,na kufichua vitu vilivyofichika.
12. “Lakini hekima itapatikana wapi?Ni mahali gani panapopatikana maarifa?
13. Hakuna mtu ajuaye thamani ya hekima,wala hekima haipatikani nchini mwa walio hai.