15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.
16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;
17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.
18. “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.
19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.
20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.