10. Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.
11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.
12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,
13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.
14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.