22. Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;mwisho wake ni kufa kwa upanga.
23. Hutangatanga kutafuta chakula,akisema, ‘Kiko wapi?’Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.
24. Taabu na uchungu, vyamtisha;vyamkabili kama jeshi la mfalme anayeshambulia.
25. Kwa sababu amenyosha mkono wake dhidi ya Mungu;akadiriki kumpinga huyo Mungu mwenye nguvu;
26. alikimbia kwa kiburi kumshambulia,huku ana ngao yenye mafundo makubwa.
27. Uso wake ameunenepesha kwa mafuta,na kiuno chake kimejaa mafuta.
28. Ameishi katika miji iliyoachwa tupu,katika nyumba zisizokaliwa na mtu;nyumba zilizotakiwa ziwe lundo la uharibifu.