18. “Nimesikia Efraimu akilalamika:‘Umenichapa ukanifunza nidhamu,kwani nilikuwa kama ndama asiyezoea nira.Unigeuze nami nitakugeukia,kwani wewe ndiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.
19. Maana baada ya kukuasi, nilitubu,na baada ya kufunzwa, nilijilaumu,nikaona haya na kuaibika,maana lawama za ujana wangu ziliniandama.’
20. “Efraimu ni mwanangu mpendwa;yeye ni mtoto wangu nimpendaye sana.Ndio maana kila ninapomtisha,bado naendelea kumkumbuka.Moyo wangu wamwelekea kwa wema;hakika nitamhurumia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
21. “Weka alama katika njia zako,simika vigingi vya kukuongoza,ikumbuke vema ile njia kuu,barabara uliyopita ukienda.Ewe Israeli rudi,rudi nyumbani katika miji yako.