1. Mwanangu, usiyasahau mafundisho yangu,bali kwa moyo wako uzishike amri zangu.
2. Maana yatakupa wingi wa siku,maisha marefu na fanaka kwa wingi.
3. Utii na uaminifu visitengane nawe.Vifunge shingoni mwako;viandike moyoni mwako.
4. Hivyo utakubalika na kusifika,mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.
5. Mtumaini Mwenyezi-Mungu kwa moyo wako wote,wala usitegemee akili zako mwenyewe.