1. Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi,ataangamia ghafla asipone tena.
2. Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.
3. Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.
4. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.
5. Mwenye kumbembeleza jirani yake,anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.