10. Ukifa moyo wakati wa shida,basi wewe ni dhaifu kweli.
11. Mwokoe mtu anayechukuliwa kuuawa bure;usisite kumwokoa anayeuawa bila hatia.
12. Usiseme baadaye: “Hatukujua!”Maana Mungu apimaye mioyo ya watu huona;yeye atakulipa kulingana na matendo yako!
13. Mwanangu, ule asali maana ni nzuri;sega la asali ni tamu mdomoni.
14. Ndivyo ilivyo hekima nafsini mwako;ukiipata utakuwa na matazamio mema,wala tumaini lako halitakuwa la bure.
15. Usivizie kama mwovu kushambulia makao ya mtu mwema,wala usijaribu kuiharibu nyumba yake,