1. Hizi ni methali za Solomoni mfalme wa Israeli, mwana wa Daudi.
2. Methali hizi zawapatia watu hekima na nidhamu; zawafanya waelewe maneno ya busara,
3. zawafanya kuwa na nidhamu, utaratibu, uadilifu, haki na kutenda kwa usawa.
4. Huwapatia wajinga werevu na vijana maarifa na hadhari.