6. “Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote.Kwa nini huwezi kuyakiri?Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya;mambo yaliyofichika ambayo hukuyajua.
7. Mambo hayo yanatukia sasa;hukupata kuyasikia kabla ya leo,hivyo huwezi kusema, ‘Aa! Nilikwisha yajua.’
8. Hujapata kamwe kuyasikia wala kuyajua;tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.Nilijua kuwa wewe ni mwenye hila,na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.
9. “Kwa heshima ya jina langu,ninaiahirisha hasira yangu;kwa ajili ya heshima yangu,ninaizuia nisije nikakuangamiza.
10. Mimi nitawajaribu lakini si kama fedha katika tanuri.Nitawajaribu katika tanuri ya taabu.