19. Waliweza kuitupa miungu yao motoni, kwa sababu haikuwa miungu kweli bali sanamu za miti au mawe zilizochongwa na mikono ya watu.
20. Sasa ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, utuokoe makuchani mwa Senakeribu, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe peke yako ndiwe uliye Mwenyezi-Mungu.”
21. Kisha Isaya mwana na Amozi, alituma ujumbe kwa Hezekia akisema, “Hivi ndivyo anavyosema Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli: Kwa kuwa umeniomba kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,
22. basi huu ndio ujumbe wangu kuhusu huyo mfalme:Mji wa Siyoni, naam, Yerusalemu,unakudharau na kukutukana.Yerusalemu, mji mzuriunakutikisia kichwa kwa dhihaka.
23. Wewe umemtukana nani?Umemkashifu nani?Umethubutu kumbeza nani kwa majivuno?Ni mimi Mungu, Mtakatifu wa Israeli!