1. Ole wao wanaotunga sheria zisizo za haki,watu wanaopitisha sheria za kukandamiza.
2. Huwanyima maskini haki zao,na kuwaibia maskini wa watu wangu maslahi yao.Wajane wamekuwa nyara kwao;yatima wamekuwa mawindo yao.
3. Je, mtafanya nini siku ya adhabu,siku dhoruba itakapowajieni kutoka mbali?Mtamkimbilia nani kuomba msaada?Mtakwenda wapi kuweka mali yenu?